
Ardhi ya Zulani EPS 4
KWENYE SEHEMU HII:
“Nitaishije mwaka mzima katika mji huu wa laana? Mwaka mmoja? Sikuweza hata kuishi siku moja salama! Vipi nikiwa mimi ndiye nitakayekuwa masikini zaidi ifikapo hiyo Siku ya Zulani? Vipi nikiwa mimi ndiye nitakayechinjwa?”
Endelea…
Habil aliinua sauti yake zaidi, akijaribu kuonyesha ujasiri ambao kiukweli
hakuwa nao..,
“Ndiyo, nitatoka! Lazima nitoke! Fungua hili lango!”
Mlinzi yule hakusumbuka hata kujibizana naye sana. Alimtazama Habil kama mdudu mdogo, kisha akamwambia..,
“Sisi huacha sherehe za Zulani ziendelee na kusimama hapa kulinda lango kwa sababu moja tu… tunajua walevi kama wewe watakuja hapa kusumbua.”
“Mimi siyo mlevi! Mimi siyo mlevi!” Habil alifoka, akisukuma mkono wa mlinzi yule kwa hasira.
Kitendo hicho kilikuwa kosa kubwa. Uso wa mlinzi ulibadilika na kuwa wa
kikatili.. Bila onyo, mlinzi huyo alirusha ngumi nzito kama jiwe iliyotua moja kwa moja kwenye uso wa Habil.. Ngumi hiyo ilimrusha Habil hewani na kumwangusha vibaya mgongoni. Damu moto ilianza kumtiririka kutoka kwenye nyusi yake ya kushoto na mdomoni.
Habil alijaribu kuinuka haraka, ingawa dunia ilikuwa ikimzunguka. Alisimama tena mbele ya mlinzi yule, akitaka kupambana. Lakini ghafla, macho yake yalitua kwenye ngao ya chuma iliyong’aa kifuani mwa mlinzi huyo, iliyokuwa kama kioo.
Habil aliiona sura yake mwenyewe kwenye ngao ile. Alishtuka. Macho yake yalipanuka kwa hofu, na mapigo ya moyo yalimwenda mbio.
Kipindi Hiki Kimefungwa
Ili kuendelea kusoma riwaya hii nzuri, tafadhali ingia kwenye akaunti yako.
Kama ni mara yako ya kwanza kufika hapa, tunakukaribisha kujisajili!

unyama sana hii hadithi👌👌